Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli aonya waliojenga mabondeni
Habari za Siasa

Rais Magufuli aonya waliojenga mabondeni

Spread the love

RAIS John Magufuli ameweka msisitizo kuwa, serikali haitatoa msaada wa aina yoyote kwa watu waliojenga mabondeni, pindi watakapopata maafa ya mafuriko. Anaripoti Hamis Mguta, Dar es Salaam … (endelea).

Akizungumza na wakazi wa Kigamboni jijini Dar es Salaam, leo tarehe 11 Februari 2020, Rais Magufuli amesema, serikali haitahangaika kusaidia mtu atakayekumbwa mafuriko mabondeni, sababu wameyataka wenyewe.

“Hakuna cha kusaidiwa, uliyatafuta mwenyewe hayo mabonde ngoja yakubondoe ili ujifunze mwenyewe. Nataka kuwaeleza ukweli ndugu zangu sitaki unafiki,” amesisitiza Rais Magufuli.

Rais Magufuli amewalaumu watu waliojenga makazi yao mabondeni na kuacha kujenga sehemu zenye miinuko, huku wakijua dhahiri kwamba maeneo hayo huwa yanakumbwa na mafuriko ya mara kwa mara kwa kuwa ni mkondo wa maji.

“Mlima upo hutaki kujenga kwenye milima unajenga kwenye bonde, nilimtuma waziri mkuu na ameshatoa maelekezo kwamba wale waliojenga mabondeni ambako wana uwezekano wa kupata maji, wahame wenyewe,” amesema Rais Magufuli na kuongeza:

“Na wala serikali haitahangaika na mtu aliyejipeleka kwenye bonde mwenyewe halafu  ishughulikie kumlisha, Uwe uko Chato,  uwe wapi huo ndio msimamo, acheni kujenga kwenye mabonde.”

Wakati huo huo, Rais Magufuli amewataka Watanzania kutumia vyema mvua, kwa kufanya shughuli za kilimo.

“Kila Mtanzania mahali alipo afanye kazi, walime mazao yanayostahili hata ukame mvua ikinyesha wewe kalime viazi, wakiwa wanafurika huko wewe unalima miogo, kunde.

Wakiwa wanafurikwa huko wewe unafanya kazi ili baadae wanapotoka kwenye mafuriko waje wale chakula chako kwa kuwatwanga pesa hayo lazima niwaleleze,” amesema Rais Magufuli.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!