Wednesday , 24 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli aongeza siku 20 usajili wa laini
Habari za Siasa

Rais Magufuli aongeza siku 20 usajili wa laini

Rais John Magufuli akisajili laini yake kwa alama ya vidole
Spread the love

RAIS John Magufuli ameongeza siku siku 20 kwa usajili wa laini za simu kwa njia ya alama za vidole kama ilivyotangazwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) na baada hapo laini zote zitazimwa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Chato … (endelea). 

Hapo awali TCRA ilitangaza siku ya mwisho ya kusajili laini zote kwa alama za vidole kuwa ni tarehe 31 Desemba, 2019 ambapo zilikuwa zimebaki siku nne kabla ya kufikia mwisho.

Rais Magufuli ametangaza ongezeko hilo la siku 20 baada ya kusajili laini yake kwa njia ya alama za vidole leo akiwa mapumzikoni Chato.

Ongezeko hilo la muda litaanzia tarehe 1 Januari, 2020 na kufikia kikomo tarehe 20 Januari, 2020 ambapo amesema baada ya hapo ambao watashindwa kusajili laini zao katika kipindi cha nyongeza laini zao zitazimwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

error: Content is protected !!