Tuesday , 19 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli amtumbua Mkurugenzi
Habari za Siasa

Rais Magufuli amtumbua Mkurugenzi

Spread the love

RAIS John Magufuli ametengua uteuzi wa mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Mpwapwa, Mohamed Maje kuanzia leo kwa kushindwa kutekeleza majukumu yake. Anaripoti Dany Tibason … (endelea).

Akitoa taarifa ya utenguzi huo mjini Dodoma, Katibu Mkuu wa Tamisemi, Alhaji Mussa Iyombe amesema kuwa Maje ameisababishia serikali hasara ikiwemo kushindwa hata kukusanya mapato ya serikali.

Utenguzi wa Maje umetokana na taarifa iliyotolewa na tume iliyoundwa kukagua utendaji wake wa kazi nakubaini kuwa ameshindwa kusimamia na kudhibiti mapato ya halmashauri hali iliyopelekea upotevu wa fedha.

“Hadi kufikia robo tatu ya mwaka wa fedha halmashauri ya wilaya ya Mpwapwa imekusanya mapato kwa asilimia 24 tu pamoja nakuwa halmashauri hiyo ni kongwe na yenye vyanzo vingi vya mapato,” amesema Iyombe.

Hatua hii imekuja baada ya Mkuu wa mkoa wa Dodoma Dk. Bilineth Mahenge kuagiza kuundwa kwa tume ya mkoa kuchunguza ubadhilifu wa fedha zaidi ya Sh. 500 milioni katika halmashauri ya wilaya ya Mpwapwa pamoja na kubaini sababu za halmashauri hiyo kuwa ya mwisho katika ukusanyaji wa mapato.

Akizungumza katika kikao cha ushauri wa mkoa (RCC) Mahenge alionyesha kusikitishwa na matokeo hayo pamoja na kuwa wilaya Kongwe nayenye vyanzo vingi vya mapato kukusanya asilimia 24 pekee ya mapato hivyo kupelekea kuchukuliwa hatua kwa watendaji wote wanaokwamisha ukusanyaji wa mapato ya ndani.

Hata hivyo Mahenge alisisitiza uadilifu kwa watendaji ikiwa ni pamoja na kupeleka mashine za kukusanyia mapato katika kata.

“Ukusanyaji wa mapato ya ndani ni muhimu sana katika halmashauri kwani ndio hutumika katika shughuli za maendeleo,ukuaji na ustawi wa halmashauri,” amesema Mahenge.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Zanzibar mbioni kuanza uchimbaji mafuta na gesi baharini

Spread the loveSERIKALI ya Zanzibar, imekamilisha mchakato wa uchimbaji wa mafuta na...

Habari za Siasa

Wizara ya afya yataja mafanikio 10 miaka mitatu Samia madarakani

Spread the loveWIZARA ya Afya imetaja mafanikio 10 iliyoyapata ndani ya miaka...

Habari za Siasa

Mbozi walilia kuwa manispaa, majimbo 3

Spread the loveHALMASHAURI ya wilaya ya Mbozi mkoani Songwe imeeleza dhamira yake...

Habari za Siasa

Wabunge waitaka TPDC kuongeza kasi ya kuunganisha wateja gesi asilia

Spread the love  KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini...

error: Content is protected !!