RAIS John Magufuli amemteua Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk. Lucas Nyaoro kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS). Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Taarifa ya uteuzi huo imetolewa leo tarehe 11 Oktoba 2018 na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu.
“Uteuzi wa Dk. Nyaoro umeanza tarehe 10 Oktoba 2018,” inaeleza sehemu ya taarifa hiyo.
Taarifa hiyo inaeleza kuwa, Dk. Nyaoro anachukua nafasi ya Hawa Magogo aliyemaliza muda wake.
Leave a comment