DAKTARI Lutengano Mwakahesya ameteuliwa na Rais John Magufuli kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri wa Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA). Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi na kusambazwa kwa vyombo vya habari na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu, uteuzi wa Dk. Mwakahesya umeanza tarehe 21 Novemba 2018.
“Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imeeleza kuwa uteuzi wa Dk. Mwakahesya umeanza tarehe 21 Novemba 2018,” inaeleza sehemu ya taarifa hiyo.
Dk. Mwakahesya aliwahi kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ambapo alistaafu mwezi Juni 2016.
Leave a comment