RAIS wa Tanzania, John Pombe Magufuli amefika nyumbani kwa Hayati Rais wa awamu ya tatu wa nchi hiyo, Benjamini William Mkapa, Masaki jijini Dar es Salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Rais Magufuli akiwa ameambatana na mkewe, Janeth wametoa mkono wa pole kwa Anna, mjane wa Mkapa, ndugu, jamaa na marafiki waliopo msibani hapo.
Mara baada ya kuwasilia, Rais Magufuli na Janeth walikwenda moja kwa moja eneo maalum lililoandaliwa kwa ajili ya kusaini kitabu cha maombolezo.
Wawilia hao baada ya kuamliza, walikwenda ndani kuwasafiri wafiwa akiwemo Anna.
Mkapa alifariki dunia usiku wa kuamkia jana Ijumaa tarehe 24 Julai 2020 katika moja ya hospitali jijini Dar es Salaam.
Mwili wa Mkapa utaagwa kwa siku tatu katika Uwanja wa Uhuru Dar es Salaam kuanzia kesho Jumapili hadi Jumanne tarehe 28 Julai 2020 kisha utasafirishwa kwenda kijijini kwake, Lupaso Mkoa wa Mtwara kwa maziko yatakayofanyika Jumatano tarehe 29 Julai 2020.
Endelea kufuatilia MwanaHALISI Online na MwanaHALISI TV kwa habari mbalimbali
Leave a comment