Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli afunga mjadala kuhusu katiba mpya
Habari za Siasa

Rais Magufuli afunga mjadala kuhusu katiba mpya

Rais John Magufuli
Spread the love

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Magufuli amefunga mjadala kuhusu mchakato wa upatikanaji wa katiba mpya, akisema kuwa hategemei kutenga fedha kwa ajili ya mchakato huo kwa sasa. Anaripoti Regina Mkonde…(endelea).

Akizungumza katika kongamano kuhusu hali ya uchumi na siasa nchini lililofanyika katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) jijini Dar es Salaam, Rais Magufuli amesema kuliko fedha kutumika katika mchakato huo, ni bora zielekezwe katika miradi ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa reli.

Aidha, amesema kama kuna watu wanataka kusaidia kutoa fedha kwa ajili ya mchakato huo, ni bora wasaidie katika ujenzi wa reli ya kisasa (Standard Gauge-SDG).

“Tusitumie hela ya kupeleka watu bungeni wakalipane posho za kila siku, tunataka hizo fedha zitumike kujenga reli, SDG, kuimarika kilimo, na ndio maana kuna mataifa makubwa katiba zao zimeundwa miaka kadhaa zilizopita. Tutakaa kubishana kupoteza pesa ‘for nothing’, huu si wakati wake,”amesema na kuongeza Rais Magufuli.

“Sitegemei kupanga hela kwa ajili ya watu kula kwa sasa hivi, na kama wako watu wanataka kutusaidia hizo fedha, watusaidie kujenga reli na SDG. lakini sikatai kusikiliza maoni ya watu, kuna ushauri tunapokea, Lakini ninachotaka kuwambia tunaenda vizuri.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari za Siasa

CCM yamkana mwenyekiti UVCCM aliyetaka wapinzani wapotezwe

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimejitenga na kauli ya mwenyekiti...

error: Content is protected !!