Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli afanya uteuzi, atengua
Habari za Siasa

Rais Magufuli afanya uteuzi, atengua

Rais John Magufuli
Spread the love

RAIS John Magufuli leo tarehe 19 Oktoba 2019 amefanya uteuzi na utenguzi wa viongozi mbalimbali. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea). 

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Gerson Msigwa, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais-Ikulu, Rais Magufuli amemteua Mathias Kabunduguru kuwa Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania. 

Taarifa hiyo imeeleza kuwa, Kabunduguru aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-TAMISEMI anayeshughulikia elimu, anachukua nafasi ya Hussein Katanga ambaye ameteuliwa kuwa Balozi.

Pia, Rais Magufuli amemteua Godfrey Mweli, kuwa Naibu Katibu Mkuu TAMISEMI anayeshughulikia elimu. Kabla ya uteuzi huo, Mweli alikuwa Mkurugenzi wa Mipango wa Wizara ya Sheria na Katiba.

Wakati huo huo, Rais Magufuli amemteua Hashim Komba, kuwa Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea akichukua nafasi ya Rukia Muwango ambaye uteuzi wake umetenguliwa.

Hali kadhalika, Rais Magufuli amemteua Hassan Rungwa, kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

Habari za Siasa

CCM yakemea ufisadi, yaipa kibarua TAKUKURU

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimekemea vitendo vya ubadhirifu wa...

Habari za Siasa

Bajeti ya Ikulu 2024/25 kuongezeka, bunge laombwa kurudhia Sh. 1.1 trilioni

Spread the love  WIZARA ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa...

error: Content is protected !!