Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Rais Kabila kushinikizwa kuachia ngazi mwaka huu
Kimataifa

Rais Kabila kushinikizwa kuachia ngazi mwaka huu

Joseph Kabila, Rais wa DR Congo
Spread the love

CHAMA cha Upinzani cha Union For Democracy and Social Progress (UDPS) cha DRC kimebainisha mpango wake wa kumshinikiza rais Joseph Kabila kuondoka madarakani, anaandika, Catherine Kayombo.

Mpango huo utahusisha migomo na kutoendelea kuitii serikali ya rais Kabila na mpango huo taayari umetangazwa na chama hicho baada ya mazungumzo ya siku mbili.

Kwa mujibu wa msemaji wa upinzani, Francois Muamba wamepanga kufanya mgomo wa kitaifa kuanzia Agosti 8 mwaka huu.

Amesema maandamano hayo yatafanyika katika jiji kuu la Kinshasa na katika majimbo 25.

Muamba alieleza kuwa ikiwa Kabila hatotangaza tarehe ya uchaguzi kufikia mwishoni mwa Septemba mwaka huu, hatatambulika tena kama rais wa Jamhusi ya Demokrasia ya Congo ifikapo Oktoba mosi mwaka huu.

Uchaguzi mkuu nchini DRC ulitakiwa kufanyika mwaka huu chini ya mkataba unaokusudia kuepusha vurugu za siasa, lakini mpaka sasa tarehe ya uchaguzi haijajulikana baada ya rais kukataa kuondoka madarakani baada ya muda wake kuisha Desemba 2016,

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

Habari MchanganyikoKimataifa

Mgombea upinzani aongoza uchaguzi wa Rais Senegal

Spread the loveMgombea wa upinzani nchini Senegal, Bassirou Diomaye Faye ameonekana kuongoza...

error: Content is protected !!