Thursday , 18 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Rais Kabila akaa pembeni Urais DR Congo
Kimataifa

Rais Kabila akaa pembeni Urais DR Congo

Joseph Kabila, Rais wa zamani wa DR Congo
Spread the love

VYAMA vinavyounda Muungano wa Common Front for Congo (FCC) umemteua aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani nchini humo, Emannuel Shadari kuwa mrithi wa Rais Joseph Kabila. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Uamuzi huo umekuja baada ya muungano huo kufanya kikao cha dharula hapo jana mjini Kinshasa ambapo walilipitisha jina la Shadari kugombea kiti cha urais kwenye uchaguzi unaotarajiwa kufanyika hivi karibuni.

Shadari amewasilisha fomu za kuwania urais kwenye Tume ya Uchaguzi Congo leo majira ya mchana.

Shadari anadaiwa kuwa na mahusiano ya karibu na Rais Kabila na aliwahi kuwa Katibu wa Kudumu wa chama tawala cha PPRD. Pia, Shadari anatajwa kwamba, alikuwa mtu wa muhimu kwenye kampeni za Rais Kabila.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

Habari za SiasaKimataifa

Rais Faye amteua aliyekuwa mfungwa mwenzie kuwa waziri mkuu

Spread the loveRais mpya wa Senegal, Bassirou Diomaye Faye, amemteua Ousmane Sonko...

error: Content is protected !!