VYAMA vinavyounda Muungano wa Common Front for Congo (FCC) umemteua aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani nchini humo, Emannuel Shadari kuwa mrithi wa Rais Joseph Kabila. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).
Uamuzi huo umekuja baada ya muungano huo kufanya kikao cha dharula hapo jana mjini Kinshasa ambapo walilipitisha jina la Shadari kugombea kiti cha urais kwenye uchaguzi unaotarajiwa kufanyika hivi karibuni.
Shadari amewasilisha fomu za kuwania urais kwenye Tume ya Uchaguzi Congo leo majira ya mchana.
Shadari anadaiwa kuwa na mahusiano ya karibu na Rais Kabila na aliwahi kuwa Katibu wa Kudumu wa chama tawala cha PPRD. Pia, Shadari anatajwa kwamba, alikuwa mtu wa muhimu kwenye kampeni za Rais Kabila.
Leave a comment