Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Rais Buhari ashinda uchaguzi Nigeria
Kimataifa

Rais Buhari ashinda uchaguzi Nigeria

Spread the love

RAIS wa Nigeria, Muhamadu Buhari ameshinda katika matokeo ya awali ya kinyang’anyiro cha uchaguzi wa urais uliofanyika Jumamosi ya tarehe 23 Februari 2019 nchini humo, kwa kupata kura milioni 15. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Kwa mujibu wa matokeo yaliyotangazwa na Tume Huru ya Kitaifa ya Uchaguzi Nigeria (INEC), Buhari amemzidi kura zaidi ya milioni 4 aliyekuwa mpinzani wake wa karibu, Atiku Aboubakar aliyeambulia kura milioni 11.

Hata hivyo, upinzani nchini Nigeria umeyakataa matokeo hayo. Katika matokeo hayo, chama cha Rais Buhari kimeshinda majimbo 19 kati ya 36 huku chama kikuu cha upinzani nchini humo cha PDP kikishinda majimbo 17.

INEC  imeahidi kuyafanyia kazi malalamiko yote ya wapinzani kabla ya kutangaza rasmi matokeo hayo ya uchaguzi.

Asilimia 35 kati ya watu 73 milioni waliojiandikisha kupiga kura walijitokeza kupiga kura katika uchaguzi huo.

Kama INEC haitabadilisha matokeo hayo, Rais Buhari aliyeingia madarakani tangu mwaka 2015 ataongoza tena Nigeria kwa muhula wa miaka minne mfululizo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!