Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Prof. Mbarawa awatoa hofu wananchi Shinyanga
Habari Mchanganyiko

Prof. Mbarawa awatoa hofu wananchi Shinyanga

Prof. Makame Mbarawa, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano
Spread the love

WAZIRI wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa, amewatoa hofu wananchi wa Kata ya Ibadakuli Manispaa ya Shinyanga kwamba hakuna mtu atakayechukuliwa ardhi yake bila kulipwa, anaandika Mwandishi Wetu

Amesema serikali haitamuonea mwananchi yeyote kwa wale ambao maeneo yao yatapitiwa na miradi mbalimbali ya uboreshaji wa miundombinu ya kiuchumi.

Waziri amesema kila mmoja atalipwa fidia kwa mujibu wa sheria ili kuipisha miradi hiyo ambayo itaisadia Tanzania kufikia kwenye uchumi wa kati mwaka (2025).

Mbarawa aliyazungumza hayo mjini Shinyanga kwenye ziara yake fupi ya ukaguzi wa miradi mbalimbali inasimamiwa na wizara anayoingoza.

Amesemma serikali imedhamiria kujenga na kufufua miundombinu yake yote ya kiuchumi, ukiwamo huo uwanja wa ndege na bandari ya Isaka wilayani Kahama, miradi ambayo itasaidia kukuza sekta ya uchumi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Puma Energy Tz: Watanzania tudumishe amani kuvutia uwekezaji

Spread the loveKAMPUNI ya Mafuta ya Puma Tanzania imewakutanisha wadau mbalimbali katika...

Habari Mchanganyiko

DAWASA waanza utekelezaji agizo la Samia

Spread the loveMamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam...

Habari MchanganyikoKimataifa

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the loveTUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais wa...

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

error: Content is protected !!