Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Prof. Lipumba: Nipo tayari kung’oka CUF
Habari za Siasa

Prof. Lipumba: Nipo tayari kung’oka CUF

Spread the love

PROFESA Ibrahim Lipumba, Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), amefungua milango kwa mwanachama mwenye uwezo kujitokeza na kugombea nafasi aliyonayo sasa. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Kiongozi huyo ameeleza leo tarehe 25 Septemba 2018 mbele ya waandishi wa habari jijini Dar es Salaama na kwamba, wakati wa kutafuta viongozi wapya unajongea hivyo wanaotaka kuwania nafasi mbalimbali ikiwa ni pamoja na uenyekiti wanapaswa kujiandaa.

Prof. Lipumba amesema kuwa, hang’ang’anii madaraka na kwamba, atakayejitokeza kuwania nafasi hiyo lazima awe na uwezo na akubalike kwa wanachama.

“Sing’ang’anii madaraka, nitaondoka lakini anayetaka nafasi hii lazima awe na uwezo pia akubalike kwa wanachama,” amesema Prof. Lipumba na kuongeza;

“CUF ni chama kinachofuata demokrasia kwa uwazi wake. Mpaka sasa hakuna mtu aliyejitokeza kutaka nafasi ya uenyekiti ambaye atapitishwa na kugombea urais kwenye Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020.”

Hata hivyo, amegusia taarifa za Katibu Mkuu wa chama hicho Maalim Seif Shariff Hamada kutaka kuhamia Chadema ambapo amesema, hata akihama, hatodhoofisha CUF Zanzibar kwa kuwa ndio ilipo mizizi ya chama hicho.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Chadema yamtaka Rais Samia aunde tume kuchunguza mauaji mgodi wa Barick

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ameombwa aunde tume huru kwa...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

error: Content is protected !!