Tuesday , 19 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Prof. Lipumba amgeuka Jaji Mutungi
Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba amgeuka Jaji Mutungi

Spread the love

MTAFARUKU mkubwa umeibuka ndani ya Kamati ya Bunge ya Katiba na Sheria, kufuatia mwenyekiti wa kamati hiyo, Mohammed Nchengerwa, kuamuru pande mbili zinazopingana ndani ya Chama cha Wananchi (CUF), kugawana muda wa kutoa maoni ndani ya kamati hiyo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Taarifa kutoka ndani ya Kamati ya Katiba na Sheria zinaeleza kuwa mara baada ya Nchengerwa kuelekeza kuwa kila upande kati ya Prof. Ibrahim Lipumba, mwenyekiti anayetambuliwa na msajili wa vyama na Maalim Seif Shariff Hamad, katibu mkuu wa chama hicho anayetambuliwa na wanachama wa chama hicho.

Kwa mujibu wa taarifa hizo, mgogoro huo ulipamba moto kufuatia baadhi ya wajumbe wa kamati hiyo, kushinikiza mwenyekiti kutoa dakika 30 kwa kila upande. Nchengerwa aligomea pendekezo hilo.

Akizungumza ndani ya kamati ya katiba na sheria, Prof. Lipumba alisema, msajili wa vyama hana nguvu ya kukikaba Chama Cha Mapinduzi (CCM), kuliko anavyoweza kuvikaba vyama vya upinzani.

Alisema,“…huyu msajili wa vyama vya siasa, ni mteule wa rais ambaye ni mwenyekiti wa chama kilichoko madarakani. Hivyo kwa vyovyote vile, anaweza kuvibana vyama vya upinzani kuliko anavyoweza kukishughulikia chama tawala.”

Alipoulizwa kuhusu nafasi ya msajili wa vyama vya siasa, katika kutatua migogoro ya ndani ya vyama hivyo, Prof. Lipumba alisema, “uwezo huo ni mdogo sana.” Alisema, migogoro ndani ya vyama, inapaswa kutatuliwa ndani ya vyama vyenyewe.

Aidha, Prof. Lipumba alidai kuwa vifungu vinavyotoa mamlaka kwa msajili wa vyama kutoa taarifa kuhusu mafunzo ya ndani ya vyama hivyo, haviwezi kutekelezeka kwa kuwa ofisi hiyo haina uwezo wa kufanya kazi hiyo.

Naye Joram Bashange, kaimu katibu mkuu wa CUF Tanzania Bara, ameiambia kamati ya katiba na sheria, kwamba muswaada uliopo ndani ya Bunge, ni mgumu kwa vyama hivyo kufanya kazi zake kama inavyotakiwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Zanzibar mbioni kuanza uchimbaji mafuta na gesi baharini

Spread the loveSERIKALI ya Zanzibar, imekamilisha mchakato wa uchimbaji wa mafuta na...

Habari za Siasa

Wizara ya afya yataja mafanikio 10 miaka mitatu Samia madarakani

Spread the loveWIZARA ya Afya imetaja mafanikio 10 iliyoyapata ndani ya miaka...

Habari za Siasa

Mbozi walilia kuwa manispaa, majimbo 3

Spread the loveHALMASHAURI ya wilaya ya Mbozi mkoani Songwe imeeleza dhamira yake...

Habari za Siasa

Wabunge waitaka TPDC kuongeza kasi ya kuunganisha wateja gesi asilia

Spread the love  KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini...

error: Content is protected !!