Tuesday , 23 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Prof. Lipumba alalamika rafu Uchaguzi Liwale
Habari za Siasa

Prof. Lipumba alalamika rafu Uchaguzi Liwale

Prof. Ibrahim Lipumba
Spread the love

PROFESA Ibrahim Lipumba, Mwenyekiti wa CUF anayetambuliwa na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, anadai kuna uwepo wa rafu katika uchaguzi mdogo wa jimbo la Liwale unaotarajiwa kufanyika tarehe 14 Oktoba 2018. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Akizungumza na wanahabari leo tarehe 9 Oktoba 2018 jijini Dar es Salaam, Prof. Lipumba amedai kuwa, kuna njama zinazofanywa na baadhi ya watumishi wa umma kwa minajili ya kukibeba Chama cha Mapinduzi CCM katika kulitwaa jimbo la Liwale kupitia uchaguzi huo.

Prof. Lipumba ameeleza kuwa, CCM inatambua kwamba CUF ina nguvu Liwale na hivyo inataka kutumia nguvu kulichukua jimbo hilo lililowazi baada ya ya aliyekuwa mbunge wake, Zubeir Kuchauka kujiuzulu na kurudi CCM.

Kufuatia madai hayo, Prof. Lipumba ameitaka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kufuatilia kwa ukaribu mwenendo wa uchaguzi huo ikiwemo maandalizi yake kwa ajili ya kuzuia njamana ili uwe wa haki.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aridhishwa utendaji mabalozi, awapa neno

Spread the loveRais wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amewapongeza mabalozi  wanaowakilisha ...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mbunge ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the loveMBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze kasi...

error: Content is protected !!