Tuesday , 19 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Prof. Kabudi aukimbia mtego wa Zitto
Habari za SiasaTangulizi

Prof. Kabudi aukimbia mtego wa Zitto

Spread the love

WAZIRI wa Katiba na Sheria, Profesa Palamagamba Kabudi ameshindwa kujibu kipengele B kwenye swali la Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe kuhusiana na idadi ya mashauri yaliyofunguliwa katika mahakama za kimataifa, ambayo serikali imeshinda na kushindwa. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Zitto leo tarehe 9 Novemba 2018 amehoji bungeni kuwa, “Je kuanzia mwaka 2000 hadi 2018 kumekuwa na mashauri mangapi dhidi ya Jamhuri ya Muungano, mangapi yameamuriwa, mangapi bado na mangapi Tanzania ilishinda.”

Lakini Prof. Kabudi hakujibu swali hilo, akisema kwamba ni la mtego na hivyo hatauingia kamwe mtego huo.

Prof. Kabudi ameeleza kuwa, serikali haita tamka chochote kuhusu kesi zilizofunguliwa kwenye mahakama za kimataifa, kwa kuwa ikitoa tamko na kuingia katika taarifa za bunge (Hansard) litahatarisha hoja za serikali katika kesi hizo.

“Masuala yote aliyoyasema, yale yaliyo katika mahakama za kimataifa serikali haitamka chochote. Nataka niwambie katika sheria za kimataifa tamko lolote nitakalolifanya hapa likaingia kwenye hansard litahatarisha hoja za serikali kwenye kesi hizo, na mtego huo uwe wa bahati mbaya au wa kutumwa sitaungia kamwe,” amesema Prof. Kabudi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Zanzibar mbioni kuanza uchimbaji mafuta na gesi baharini

Spread the loveSERIKALI ya Zanzibar, imekamilisha mchakato wa uchimbaji wa mafuta na...

Habari za Siasa

Wizara ya afya yataja mafanikio 10 miaka mitatu Samia madarakani

Spread the loveWIZARA ya Afya imetaja mafanikio 10 iliyoyapata ndani ya miaka...

Habari za Siasa

Mbozi walilia kuwa manispaa, majimbo 3

Spread the loveHALMASHAURI ya wilaya ya Mbozi mkoani Songwe imeeleza dhamira yake...

Habari za Siasa

Wabunge waitaka TPDC kuongeza kasi ya kuunganisha wateja gesi asilia

Spread the love  KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini...

error: Content is protected !!