Tuesday , 19 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Prof. Kabudi: Afrika hakuna kama Mwl. Nyerere
Habari za Siasa

Prof. Kabudi: Afrika hakuna kama Mwl. Nyerere

Spread the love

WAZIRI wa Mambo ya Nje ya Nchi, Prof. Palamagamba Kabudi amesema, hakuna kiongozi aliyefanya makubwa Afrika zaidi ya Rais wa Awamu ya Kwanza, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Anaripoti Hamis Mguta … (endelea).

Kabudi ametoa kauli hiyo leo tarehe 21 Agosti 2019, wakati akitoa shukrani kwa waandishi wa habari kutokana na ushiriki wao katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC).

Amesema, miongoni mwa viongozi ambao waliwahi kusema hadharani kuwa kiongozi huyo ni mkubwa kuliko wote ni Rais wa Uganda, Yowel Kaguta Museveni.

“Katika nyakati hizi, hakuna kiongozi mkubwa wa Bara la Afrika zaidi ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, hakuna nchi yoyote iliyo kusini ambayo haikusaidiwa na Tanzania kupata Uhuru au kujitegemea,” amesema.

Ameeleza, moja ya sababu ambayo ameitoa Rais wa Afrika Kusini, Matamela Cyril Ramaphosa kuhusu maendeleo ya Tanzania alipokwenda mkoani Morogoro kwa jailli ya ziara ya kutembelea makaburi ya mashujaa waliopigania uhuru wa nchi hiyo, ni kuwa maendeleo yanayoonekana sasa Tanzania, yamechelewa kwasababu ya kusaidia nchi zingine kwa kutumia rasilimali zake.

“Rais Ramaphosa alisema, kule mazimbu kwamba Tanzania ilifika hatua ya kubomoa madaraja yake na kuharibu barabara zake ili Wareno wasivamie nchi hiyo.

“Sehemu mbalimbali za Tanzania ni mahala viongozi wengi wa Afrika wamepata mafunzo yao,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Zanzibar mbioni kuanza uchimbaji mafuta na gesi baharini

Spread the loveSERIKALI ya Zanzibar, imekamilisha mchakato wa uchimbaji wa mafuta na...

Habari za Siasa

Wizara ya afya yataja mafanikio 10 miaka mitatu Samia madarakani

Spread the loveWIZARA ya Afya imetaja mafanikio 10 iliyoyapata ndani ya miaka...

Habari za Siasa

Mbozi walilia kuwa manispaa, majimbo 3

Spread the loveHALMASHAURI ya wilaya ya Mbozi mkoani Songwe imeeleza dhamira yake...

Habari za Siasa

Wabunge waitaka TPDC kuongeza kasi ya kuunganisha wateja gesi asilia

Spread the love  KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini...

error: Content is protected !!