Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Polisi watimiza agizo la Mahakama, Halima Mdee mbaroni
Habari za Siasa

Polisi watimiza agizo la Mahakama, Halima Mdee mbaroni

Halima Mdee, Mbunge wa Kawe akiwa mahakamani Kisutu
Spread the love

HALIMA Mdee, Mbunge wa Kawe (Chadema) anashikiliwa na Jeshi la Polisi katika kituo cha Oysterbay, kwa amri ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo tarehe 16 Novemba 2019 na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kupitia ukurasa wake wa Twitter, Mdee anashikiliwa baada ya kujisalimisha kituoni hapo.

Taarifa hiyo inaeleza kuwa, Mdee alikwenda katika kituo cha polisi cha Oysterbay, kwa ajili ya kumuona Mkuu wa Upelelezi wa Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni (RCO).

Hata hivyo, Polisi wamesema watamshikilia Mdee hadi Jumanne ijayo ya tarehe 19 Novemba 2019, watakapomfikisha mahakamani.

Jana tarehe 15 Novemba 2019 Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, iliamuru Mdee pamoja na wabunge wengine watatu wa Chadema, kukamatwa kutokana na kushindwa kufika mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili, bila ya kutoa taarifa.

Amri hiyo ilitolewa na Hakimu Mkazi Mkuu wa mahakama hiyo, Thomas Simba.

Wabunge wengine ambao mahakama imeamuru wakamatwe ni Mchungaji Peter Msigwa, Mbunge wa Iringa Mjini, John Heche, Mbunge wa Tarime Vijijini na Ester Bulaya, Mbunge wa Bunda Mjini.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

Habari za Siasa

CCM yakemea ufisadi, yaipa kibarua TAKUKURU

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimekemea vitendo vya ubadhirifu wa...

Habari za Siasa

Bajeti ya Ikulu 2024/25 kuongezeka, bunge laombwa kurudhia Sh. 1.1 trilioni

Spread the love  WIZARA ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa...

error: Content is protected !!