Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Polisi watatu wafariki ajalini Rufiji
Habari Mchanganyiko

Polisi watatu wafariki ajalini Rufiji

Spread the love

ASKARI watatu wameripotiwa kufariki katika ajali ya gari ya Polisi mkoa wa kipolisi Rufiji iliyotokea baada ya gurudumu la nyuma la gari hiyo kupasuka na kusababisha gari kupinduka. Anaripoti Hamis Mguta … (endelea).

SACP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini leo amewaambia waandishi wa habari kuwa ajali hiyo imetokea jana tarehe 25 Julai 2019 majira ya saa saba mchana katika kijiji cha Kilimahewa wilayani Mkuranga, Rufiji. 

Gari hilo Toyota Land Cruiser lenye namba za usajili PT. 3822 lilikuwa likitokea Ikwiriri kuelekea Kijiji cha Mwalusembe, lilipasuka gurudumu moja la nyumba upande wa kulia na kusababisha kupinduka.

“Askari waliofariki kwenye ajali hiyo ni aliyekuwa Afisa Mnadhimu Rufiji, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Issah Bukuku na Inspekta Esteria wa Ofisi ya Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Kipolisi Rufiji pamoja na namba G.1132 PC Lameck wa Kikosi cha kutuliza ghasia (FFU) mkoani humo,” amesema.

Waliojeruhiwa ni F.7167 PC Ibrahim ambaye ndio alikuwa dereva wa gari hilo pamoja na F.7651 PC Mgusi wa ofisi ya Kamanda wa Polisi Rufiji.

SACP Misime amesema kuwa majeruhi wote wawili wamefikishwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Dar es Salaam kwa ajili ya matibabu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

Habari Mchanganyiko

NMB yafuturisha Dar, Majaliwa azitaka Serikali za Mitaa, Taasisi zijifunze kwao

Spread the loveBENKI ya NMB imewafuturisha wateja wake walio kwenye Mfungo wa...

error: Content is protected !!