Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Polisi wampiga risasi mtuhumiwa utekaji watoto Arusha
Habari Mchanganyiko

Polisi wampiga risasi mtuhumiwa utekaji watoto Arusha

Samson Petro kijana aliyeuwawa na Polisi. Picha ndogo Kamanda wa Arusha, Charles Mkumb
Spread the love

MTUHUMIWA aliyekuwa ameshikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoani Arusha kwa kuhusika na utekaji na mauaji ya watoto wawili Maureen na Ikram amefariki dunia kwa kupigwa risasi wakati akijaribu kutoroka mikononi mwa polisi, anaandika Irene David.

Kijana huyo anayejulikana kwa jina la Samson Petro, alikiri kuhusika na matukio mbalimbali ya utekaji wa watoto katika mikoa mbalimbali ikiwemo Arusha na Geita kwa lengo la kujipatia fedha.

Samson alipigwa risasi wakati akijaribu kutoroka kituo cha polisi na mwili wake upo katika hospitali ya mkoa wa Arusha Mount Meru.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha, Charles Mkumbo , amekiri kutokea tukio hilo na kwamba mtuhumiwa alipigwa risasi baada ya kujaribu kuwakimbia polisi alipokuwa amepelekwa kuwaonyesha mtu anayedaiwa kuwa walikuwa wanashirikiana katika utekaji huo wa watoto.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

error: Content is protected !!