Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Polisi walikoroga Ruvuma, wazuia vikao vya ndani vya Chadema
Habari za Siasa

Polisi walikoroga Ruvuma, wazuia vikao vya ndani vya Chadema

Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema
Spread the love

JESHI la Polisi mkoani Ruvuma limekizuia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kufanya mikutano ya ndani, anaandika Irene David.

Katazo hilo limekuja siku chache baada ya viongozi waandamizi wa chama waliokuwa mkoani humo akiwamo Katibu Mkuu, Vicent Mashinji kushikiliwa na vyombo vya usalama kwa madai kwamba wanatumia lugha za kashfa na matusi kwa viongozi wa umma.

Kwa mujibu wa barua ya Kamanda wa Polisi iliyotumwa kwa Mkuu wa Mkoa huo, IGP  na Ofisa Usalama wa Taifa, ni marufuku viongozi hao kufanya mikutano ya ndani.

Kamanda wa Polisi wa mkoa huo, Gemini Mushy, amesema viongozi hao wa Chadema wanafanya shughuli zao kinyume cha sheria ya polisi sura 322 fungu 43(4).

Alisema sheria hiyo unawapa polisi mamlaka ya  kuchukua  hatua za  kuzuia shughuli kama hizo.

Kamanda huyo katika taarifa amesema viongozi hao wataruhusiwa pale  jeshi la polisi litakapojiridhisha kwamba wanafuata maelekezo yanayoendana na vikao vya ndani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!