Wednesday , 24 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Polisi wakiri kumshikilia Mtumishi LHRC, atuhumiwa kosa la jinai
Habari Mchanganyiko

Polisi wakiri kumshikilia Mtumishi LHRC, atuhumiwa kosa la jinai

Lazaro Mambosasa, Kamanda wa Polisi Dar es Salaam
Spread the love

JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limekiri kumshikilia Tito Magoti, Afisa Program wa Kituo cha Sheria  na Haki za Binadamu ( LHRC ),kwa tuhuma za makosa ya jinai. Anaripoti Regina Mkonde…(endelea)

Taarifa hiyo imetolewa leo tarehe 20 Desemba 2019, na SACP Lazaro Mambosasa, Kamanda wa Kanda hiyo.

Hata hivyo, Mambosasa hakuweka bayana aina ya makosa ya jinai, yanayomkabili Magoti, pamoja na watu wengine watatu, ambao wamekamatwa na polisi, leo majira ya saa tano asubuhi, maeneo ya Mwenge, jijini Dar es Salaam.

Kamanda Mambosasa amesema Magoti na wenzake, wanahojiwa na Jeshi la Polisi, na kwamba uchunguzi dhidi ya tuhuma zinazowakabili ukikamilika, watafikishwa mahakamani.

“Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam linamshikilia Magoti, Mkazi wa  Ubungo Kibo , pamoja na watu wengine watatu kwa uchunguzi na mahojiano zaidi. Wanaendelea kuhojiwa kwa tuhuma za makosa ya jinai,” ameeleza Kamanda Mambosasa.

https://youtu.be/uM77yTNOPas

Hata hivyo, Kamanda Mambosasa amesema taarifa ya kwamba Magoti ametekwa na watu wasiojulikana si za kweli, kwa kuwa yuko katika mikono salama ya Jeshi la Polisi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the loveMADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaahidi kuendelea kuunga mkono Serikali za Mitaa

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya...

Habari Mchanganyiko

Watuhumiwa 12 wa kilo 726.2 za dawa za kulevya wafikishwa mahakamani

Spread the love  WATUHUMIWA watatu wamefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kibaha Mkoani...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!