Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Polisi Mbeya wamsaka dereva wa lori
Habari Mchanganyiko

Polisi Mbeya wamsaka dereva wa lori

Kamanda wa Polisi mkoa wa Mbeya, Ulrich Matei
Spread the love

JESHI la Polisi mkoani Mbeya linamsaka dereva wa lori la mafuta linalomilikiwa na Kampuni ya Mafuta ya Oil Com, baada ya lori hilo kukutwa limebeba vipodozi vilivyopigwa marufuku kuingia nchini. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Hatua hiyo ya Jeshi la Polisi Mbeya imekuja baada ya kukamata lori hilo maneneo ya Mbarali jijini Mbeya, likiwa limebeba katoni mbili za pome kali pamoja na katoni 15 za vipodozi.

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari iliyotolewa leo tarehe 9 Oktoba 2018, Kamanda wa Polisi mkoa wa Mbeya, Ulrich Matei, ameeleza kuwa lori hilo limekamatwa jana majira ya saa nane mchana likitokea nchini Zambia.

“Lori hilo lenye namba za usajili T 233 CXL limekamatwa na polisi eneo la Mbarali jijini hapa, jana saa nane mchana, likitokea nchini Zambia,” amesema Kamanda Matei.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

error: Content is protected !!