Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Polisi, Dawasco, Tanesco kuanzisha msako mkali
Habari Mchanganyiko

Polisi, Dawasco, Tanesco kuanzisha msako mkali

Spread the love

JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam kwa kushirikiana na Tanesco, Dawasco na kampuni mbalimbali za simu za mkononi limeanzisha msako dhidi ya watu wanaohujumu miundombinu ya mashirika hayo. Anaripoti Khalifa Abdallah … (endelea).

Akizungumza na waandishi wa habari Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amesema kuanzia tarehe 27 Agosti mwaka huu, litafanya operesheni hiyo kali itaanza kuhakikisha mtandao wa wizi huo unaisha.

“Kumekuwa na wimbi kubwa la watu kujiunganishia maji safi kutoka kwenye mabomba ya DAWASCO bila kufuata utaratibu, pia wanaojiunganishia umeme kinyume na utaratibu, kuiba mafuta ya transformer na kuiba betri kwenye minara ya kampuni za simu hapa jijini Dar es Salaam,” amesema.

Aidha Mambosasa amesema Jeshi la Polisi kuanzia sasa linawataka watu wote wanaojihusisha na uhalifu huo kuacha mara moja  na kujisalimisha wenyewe  katika vituo vya Polisi au katika mashirika na kampuni hizo kabla ya kuanza kwa oparesheni hiyo kali, na watakaokaidi agizo hili watakamatwa na kufunguliwa mashtaka ya uhujumu uchumi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

error: Content is protected !!