Tuesday , 23 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Polisi Dar mguu sawa sikukuu ya Eid
Habari Mchanganyiko

Polisi Dar mguu sawa sikukuu ya Eid

Spread the love

JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewahakikishia  hali ya usalama na amani wakazi, wananchi wa jiji la Dar es Salaam katika kipindi chote cha sikukuu ya Eid inayotarajiwa kuwa kati ya Jumapili wiki hii au Jumatatu ijayo, anaandika Yasinta Francis.

Lucas Mkondya, Kaimu Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam amesema kuwa askari wa jeshi hilo wamejipanga vyema kuhakikisha wananchi wa jiji la Dar es Salaam wanasherehekea sikukuu hiyo kwa kwa amani na utulivu pasipo bugudha za wahalifu.

“Uzoefu unaonesha kuwa, mara nying kipindi cha sikukuu kama hii watu wenye nia ovu hujiandaa kufanya vitendo vya kihalifu, ndiyo maana tumejipanga kukabiliana na aina yoyote  ya uhalifu kwa kuzuia au kuwatia nguvuni wote watakaoshiriki vitendo vya uvunjifu wa sheria,” amesema.

Kamanda Mkondya amesema polisi watafanya doria za masaa 24 katika maeneo yote ya jiji la Dar es Salaam hasa maeneo yenye korofi na yenye rekodi au viashiria vya uhalifu.

“Pia kutakuwa na doria katika maeneo ya misikiti, kumbi za starehe na maeneo yenye mikusanyiko mikubwa ya watu na tutatumia taarifa za kiintelijensia ili kuwabaini wahalifu wanaopanga kufanya matukio ya uhalifu.

“Tutaimarisha vikundi vya ulinzi shirikishi ili kuhakikisha maeneo yote hatarishi yanadhibitiwa,” amesema Kamanda Mkondya.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari Mchanganyiko

DC ampongeza Dk. Rose Rwakatare kwa kusaidia waathirika wa mafuriko Mlimba

Spread the loveMWENYEKITI wa Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dk.  Rose Rwakatare...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mbunge ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the loveMBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze kasi...

error: Content is protected !!