Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Polisi Dar: Kipigo kwa walemavu kilikuwa halali
Habari Mchanganyiko

Polisi Dar: Kipigo kwa walemavu kilikuwa halali

Lucas Mkondya, Kaimu Kamishna wa Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam
Spread the love

SIKU tatu baada Jeshi la Polisi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam kuonekana wakiwaadhibu watu wenye ulemavu waliokuwa wakifanya maandamano kupinga kuzuiwa kuingia katikati ya jiji, polisi wamesema, ulemavu si kibali cha kuvunja sheria, anaandika  Yasinta Francis.

Lucas Mkondya, Kamanda  wa  Polisi  Kanda  Maalum Dar es Salaam amesema nguvu iliyotumiwa na polisi haikuwa kubwa na kwamba walemavu hao walifunga njia na kuvamia ofisi ya mkurugenzi wa manispaa ya Ilala na walikaidi maagizo ya jeshi hilo.

“Ulemavu si kibali cha kuvunja sheria. Hawa walemavu walifanya makosa, walivamia ofisi ya manispaa, wakafunga njia na tulipowasihi wafungue njia na wateue viongozi wa kushughulikia matatizo yao walikaidi.

“Ikabidi tutumie nguvu kidogo tu kwenda kuwaondosha. Walemavu wajaribu kuheshimu sheria za nchi kwani sheria za nchi ni lazima zisimamiwe. Polisi tukiona sheria zinavunjwa lazima tusimamie, ambaye hataki kukumbana na mkono wa polisi basi atii sheria za nchi,” amesema Kamanda Mkondya.

Amekanusha taarifa kuwa nguvu iliyotumika kuwadhibiti walemavu hao ilikuwa ni kubwa kupitiliza, pamoja na madai ya kuwepo kwa uvunjifu wa haki za binadamu.

Tukio la kukamatwa na kupigwa kwa walemavu lilitokea tarehe 16 Juni, 2017. Pamoja na mambo mengine lakini walemavu hao walikuwa wakipinga agizo la serikali la kuwataka walemavu kutoingia katikati ya jiji wakiwa na pikipiki za miguu mitatu na  kuegesha  katikati  ya jiji.

Madai  hayo  ya  walemavu  yanalindwa  na  Mkataba  wa  Kimataifa  wa Haki za watu wenye Ulemavu Ibara  ya 9 wa mwaka 2006.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

error: Content is protected !!