Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Polisi afumwa na bangi, gongo, viroba
Habari Mchanganyiko

Polisi afumwa na bangi, gongo, viroba

Spread the love

JESHI la Polisi nchini Tanzania, limemtimua kazi ofisa wake kwa kukutwa na bangi, gongo, viroba pamoja na kujiunganishia umeme kinyume cha utaratibu. Anaandika Mwandishi Wetu, Arusha…(endelea).

Polisi huyo aliyetambulika kwa jina la F.1445 Koplo William, alifukuzwa baada ya Kenan Kihongosi, Mkuu wa Wilaya ya Arusha kuvamia nyumbani kwa askari huyo.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Alhamisi tarehe 7 Januari 2021, Salum Hamduni, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha amesema, Kihongosi alivamia nyumbani kwa askari wake baada ya kupata taarifa kutoka kwa wananchi.
Kamanda huyo amesema, mkuu huyo wa wilaya na timu yake walipofika nyumbani kwa Koplo William, miongoni mwa mambo waliyobaini ni pamoja na kujiunganishia umeme kinume cha sheria.

Salumu Hamduni, RPC Arusha

Pia, walikuta mafuta ya dizeli lita 85, gongo lita tano, misokoto ya bangi 20 na viroba vilivyokatazwa na serikali boksi 84 ambavyo vimekatazwa na serikali pia chupa zenye konyagi tisa.

Amesema, uvamizi huo ulifanywa tarehe 5 Januari 2021, saa tatu usiku katika Mtaa wa Muriet, Kata ya Sokoni One.

Kamanda Hamduni amesema, askari wengine watatu walikamatwa kwa tuhuma za rushwa baada ya kushawishi kutaka rushwa kutoka kwa Sammy Mollel, mmiliki wa Kampuni ya Gems and Rocks Venture.

Na kwamba, askari hao walimteka Lucas Mdeme, Meneja wa Kampuni ya kuuza madini ya Crown Lapidary, Arusha wakimtaka awape Sh. 30 milioni.

Askari waliohusika katika tukio hilo ni Gasper Paul (H.125) kutoka Kitengo cha Intelijensia Makao Makuu, Heavenlight Mushi (G.5134) kutoka Kitengo cha Intelijensia Mkoa wa Kinondoni na Bryton Murumbe (H.1021) aliyekuwa Polisi Kazi za Kawaida Dodoma.

Kamanda Hamduni amesema, upelelezi wa kesi zao umekamilika na sasa, majalada yao yanapelekwa kwenye ngazi nyingine kwa hatua zaidi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!