JESHI la Polisi nchini, limekataza kufanyika maandamano ya tarehe 9 Aprili 2019 yaliyopangwa na Ngome ya Vijana wa Chama cha ACT-Wazalendo. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).
Wakati jeshi hilo likikataza maandamano hayo, ACT-Wazalendo wameeleza kuwa, watafanya kwa kuwa ni haki yao ya kikatiba.
Tarehe 6 Aprili 2019 Isack Nyasilu, Katibu wa Ngome ya Vijana ya ACT-Wazalendo, alitangazakufanya maandamano kesho tarehe 9 Aprili, 2019 kupinga azimio la bunge la kutofanya kazi na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Profesa Mussa Assad.
Taarifa hiyo ya zuio la polisi imewekwa leo tarehe 8 Aprili 2019 katika ukurasa wake wa Twitter wa ACT-Wazalendo ikieleza kuwa, polisi wamepiga marufuku maandamano hao.
Tumepokea taarifa RPC wa Dodoma amezuia maandamano ya Ngome,Jumuia na Mabaraza ya Vijana ya Vyama vya siasa.
Tunapenda kumjulisha kuwa sisi kama Social Auditors tunahaki ya kuhoji na kusimama na CAG,
Tunaendelea na Maandamano kama yalivyopangwa kwa kuwa ni haki yetu ya Kikatiba.— NGOME YA VIJANA TAIFA_Official (@NgomeyaVijana) April 8, 2019
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Kamanda wa Polisi mkoani Dodoma, Gilles Muroto amezuia maandamano hayo.
Licha ya zuio hilo, Ngome ya Vijana ya ACT-Wazalendo imesema, utaratibu wake katika kushiriki maandamano hayo uko pale pale.
“Tumepokea taarifa RPC wa Dodoma kuwa amezuia maandamano ya Ngome, Jumuiya na Mabaraza ya Vijana ya Vyama vya siasa.
“Tunapenda kumjulisha kuwa, sisi kama Social Auditors tunahaki ya kuhoji na kusimama na CAG, tunaendelea na maandamano kama yalivyopangwa kwa kuwa, ni haki yetu ya kikatiba,” inaeleza taarifa ya Ngome ya Vijana ya ACT-Wazalendo.
Taarifa hiyo imeeleza kuwa, utaratibu wa usafiri wa kutoka Dar es Salaam, Morogoro, Singida na Iringa kwenda Dodoma kushiriki maandamano ya tarehe 9/4/19 upo kama ulivyopangwa.
Leave a comment