Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Polepole: Watu mashuhuri wanaokufa ni wa CCM
Habari Mchanganyiko

Polepole: Watu mashuhuri wanaokufa ni wa CCM

Spread the love

HUMPHREY Polepole, Katibu wa Itikati na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) amesema, watu wengi mashuhuri wanaokufa huwa wanachama wa chama hicho. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Akitoa salamu za pole kwenye kwenye shughuli ya kuuaga mwili wa Dk. Reginald Abraham Mengi iliyofanyika katika Viwanja vya Karimjee, jijini Dar es Salaam leo tarehe 7 Mei 2019, Polepole amesema CCM ina bahati ya kuwa na watu maarufu.

“Kwenye chama chetu tuna bahati, watu wote mashuhuri wanaokufa ni wana CCM, Mzee Menegi wala hakujificha, alikuwa rafiki wa Rais Magufuli (Rais John Magufuli,” amesema.

Kwenye salamu zake kwa wafiwa, Polepole amewataka kutokata tamaa na kuwa imara kama alivyokuwa Dk. Mengi.

“Tusikate tamaa, tupambane kama mtu, taasisi na taifa. Dk. Mengi ametufundisha kutafuta. Alikuwa mtu madhubuti, makini na ambaye ametuonesha kwamba, inawezekana,” amesema.

Amesema, baada ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 ndani ya chama hicho hakukuwa sawa kidogo na kwamba, ushauri wake umesaidia kuweka mambo sawa.

Ameeleza kuwa, ni vizuri Watanzania wakaendeleza dhamira ambayo Dk. Mengi aliyoonesha kama mfano huku akisisitiza kuendelea kuwekwa vizuri mazingira ya sekta binafsi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

Habari Mchanganyiko

NMB yafuturisha Dar, Majaliwa azitaka Serikali za Mitaa, Taasisi zijifunze kwao

Spread the loveBENKI ya NMB imewafuturisha wateja wake walio kwenye Mfungo wa...

error: Content is protected !!