Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Polepole aondoka Z’bar kichwa chini
Habari za Siasa

Polepole aondoka Z’bar kichwa chini

Humphrey Polepole, Aliyekuwa Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM
Spread the love

ZANZIBAR ni ngumu. Hivi ndivyo unavyoweza kusema baada ya viongozi wa juu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kuondoka patupu visiwani humo. Anaripoti Jabir Idrissa, Zanzibar … (endelea).

Mbwembwe na maneno ya kijasiri ambayo hutolewa na Dk. Bashiru Ally, Katibu Mkuu pia Humphrey Polepole, Mwenyekiti wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho wanapopokea ‘wahamiaji,’ safari hii hazijasikika.

Licha ya Dk. Bashiru kufanya ziara visiwani Zanzibar miezi michache iliyopita na kuondoka kama alivyokwenda, Polepole naye ametoka kimya kimya Pemba.

Tayari viongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, wanaonesha shangwe kwa wakazi wa visiwa hivyo, kusimama imara bila kuhama na kujiunga na CCM kama ilivyozoeleka Tanzania Bara.

Kwa mujibu wa Salimu Bimani, Mwenyekiti wa Kamati ya Itikikadi, Uenezi na Mawasiliano kwa Umma wa ACT-Wazalendo, Polepole ametoka Pemba hivi karibuni. Hakupokea mgeni yeyote.

Katika ukurasa wake wa Twitter leo tarehe 26 Februari 2020, Bimani amesema Polepole alikwenda visiwani humo kwa kishindo, lakini ameondoka kimya kimya.

“Hongera sana Mwenezi Mwenzangu Polepole, wazee wa kwetu walisema “siasa sio usheza,” umekwenda Pemba kwa kishindo umeondoka bila ya kuagwa.

“Pemba peremba Ukienda na Joho Utarudi na Kilemba” CCM Imeshakufa Pemba na Unguja,” ameandika Bimani.

Bimani ameeleza kuwa, kitendo cha Polepole kuondoka patupu Zanzibar kinaashiria kwamba, CCM imepoteza ushawishi visiwani humo.

“Mwenezi Mwenzangu mbona umeondoka Pemba kimya kimyaa!” Pemba Peremba Ukienda na Joho Utarudi na Kilemb, hivi hujui kuwa CCM imeshatalakiwa zamani Pemba na Unguja, haya kuwa uyaone. Wazee wa kwetu walisema zamani kuwa “Siasa sio Usheza.”  Tukutane (Oktoba) Oct 2020 tukiwa na Tume Huru,” ameandika Bimani.

Written by
Jabir Idrissa

+255 774 226248

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!