ALIYEKUWA mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi ya Chama cha Wananchi (CUF), Julius Mtatiro, ameondoka chama hicho na kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM). Anaripoti Saed Kubenea … (endelea).
Akitangaza uamuzi wake huo mbele ya waandishi wa habari, Mtatiro alisema, ameamua kuchukua hatua hiyo kwa kuwa anataka kuwa “balozi bora wa Rais John Magufuli, ndani na nje ya nchi.”
Kuondoka kwa Mtatiro, kunalenga moja kwa moja kumdhoofisha “jabari la kisiasa” Visiwani, Maalim Seif Shariff Hamad.
Maalim Self amekuwa mwiba mkali kwa CCM na serikali yake, Tanzania Bara na Zanzibar – kabla na baada ya mfumo wa vyama vingi nchini.
Uchambuzi kamili juu ya kuondoka kwa Mtatiro, athari zake na uimara wa Maalim Self, soma MwanaHALISI Online kesho.
Leave a comment