Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Pigo Pwani, Katibu Chadema amfuata Sumaye
Habari za Siasa

Pigo Pwani, Katibu Chadema amfuata Sumaye

Casmir Mabina, Katibu wa Chadema Kanda ya Pwani
Spread the love

MAZINGIRA ya demokrasia goigoi ndani ya Chama cha Demokrasia na Mamendeleo (Chadema), yamemkimbiza Casmir Mabina, Katibu wa Chadema Kanda ya Pwani. Anaripoti Hamis Mguta … (endelea).

Mabina ametangaza uamuzi huo leo tarehe 4 Desemba 2019, jijini Dar es Salaam, saa chache baada ya Fredrick Sumaye, aliyekuwa mwenyekiti wa kanda hiyo, kutangaza kujiondoa Chadema.

Ingawa hakueleza sababu za kujiuzulu wadhifa huo, Mabina amesema ameamua kujiuzulu kutokana na mazingira ya siasa yaliyokuwepo ndani ya Chadema.

“Kutokana na mazingira ya kisiasa yalivyo ndani ya Chadema, leo nimewasilisha barua yangu ya kujiuzulu. Kwamba kwa mazingira haya lazima nijiuzluzu,” ameeleza Mabina.

Mabina amesema, atabaki kuwa mwanachama wa kawaida wa Chadema.

“Nimeeleza nitabakia kuwa mwanachama wa kawaida katika chama change, kwenye tawi langu. Labda kama kutakuwa na mambo mengine yatakayojitokeza,” amesema Mabina

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!