PAPA Francis, Kiongozi Mkuu wa Kanisa Katoliki duniani amesema, dunia haiwezi kupuuza ubaguzi wa rangi na kutengwa kwa watu. Inaripoti Mitandao ya kimataifa …(endelea)
Pia, ametoa wito wa kusimamisha uharibifu akisema, si sahihi na haivumiliki kutenda vurugu na uharibifu.
“Hatuwezi kujitia upofu kuhusu ubaguzi na kutengwa, lakini si sahihi kuendesha vurugu na uharibifu,” amesema Papa Francis leo tarehe 3 Juni 2020 akieleza hisia zake kuhusu kinachoendelea nchini Marekani.
Akitumia lugha ya Kiingereza amesema, analiombea Mungu taifa hilo lirejee katika hali ya amani na umoja.
Pia, amesisitiza umuhimu wa kuwa pamoja na kufikia muafaka kuhusu kile kilichotendeka ndani ya taifa hilo.
Taarifa za mchana huu leo Jumatano zinaeleza, maandamano nchini humo yanazidi kushika kasi huku vitendo vya uporaji na vurugu vikipungua kwa kiasi kikubwa.
Taarifa zinaeleza, miji ya Houston, Texas kumekuwa na maandamano makubwa zaidi kuwahi kutokea. Maeneo mengine yameanzisha maandamano kupinga mauaji ya Floyd.
Houston, eneo ambalo Floyd atazikwa, meya wa jiji hilo, Sylvester Turner amewaambia waandamanaji “Floyd hakufa bure,” kwamba ameacha somo Marekani.
Waandamaji katika Miji ya Los Angeles, Philadelphia, Atlanta na Seattle wameendelea kuvutana na vyombo vya usalama huku kukiwa hakuna dalili ya kupoa kwa maandamano hayo.
Matumizi makubwa ya gesi na maji kuwasha yameripotiwa kwenye miji ya Seattle, Portland na Atlanta
Leave a comment