Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Papa aridhia Kadinali Pengo kustaafu, Askofu Ruwa’ichi ampokea
Habari Mchanganyiko

Papa aridhia Kadinali Pengo kustaafu, Askofu Ruwa’ichi ampokea

Spread the love

OMBI la Kadinali Polycarp Pengo, Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam kung’atuka madarakani, limeridhiwa na Papa Francisko. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Papa Francisko amebariki ombi la Kadinali Pengo kuondoka madarakani alipokuwa kwenye maadhimisho ya Sherehe ya Bikira Maria Kupalizwa Mbinguni.

Hata hivyo, Papa Francisko amemteua Askofu mkuu mwandamizi, Yuda Thaddeus Ruwa’ichi wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam kuchukua nafasi ya Kadinali Pengo kuanzia sasa.

“Katika maadhimisho ya Sherehe ya Bikira Maria Kupalizwa Mbinguni, mwili na roho, tarehe 15 Agosti 2019, Baba Mtakatifu Francisko ameridhia ombi la Kardinali Polycarp Pengo, Askofu mkuu wa Jimbo kuu la Dar es Salaam, Tanzania la kung’atuka kutoka madarakani,” imeeleza taarifa ya Padre Charles Kitima, Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC).

Hivi karibuni, Kadinali Pengo katika maadhimisho ya kumbukumbu ya miaka 75 tangu kuzaliwa kwake, aliwaambia watu wa Mungu Jimbo Kuu la Dar es Salaam kwamba, anasubiria wakati wowote kumtii Baba Mtakatifu Francisko atakapomwambia kupumzika katika utume wa Kiaskofu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Gardner Habash wa Clouds Fm afariki dunia

Spread the loveALIYEKUWA mtangazaji wa kipindi cha Jahazi kinachorushwa na kituo cha...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

error: Content is protected !!