Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Pambalu ajitosa uenyekiti BAVICHA
Habari za Siasa

Pambalu ajitosa uenyekiti BAVICHA

Bendera ya Chadema
Spread the love

JOHN Pambalu, Diwani Kata ya Butimba jijini Mwanza, ametangaza nia ya kugombea uenyekiti wa Baraza la Vijana la Chadema (Bavicha). Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Pambalu ambaye ni Makamu Mwenyekiti Bavicha, ametangaza nia hiyo leo tarehe 30 Novemba 2019, baada ya kurejesha fomu ya kugombea uenyekiti wa baraza hilo, kwenye Ofisi za Chadema, zilizoko jijini Dar es Salaam.

“Nimeamua kuutangazia umma wa Watanzania na dunia kwa ujumla kwamba, nimetia nia ya kugombea uenyekiti wa Bavicha.  Uamuzi umekuja baada ya kujitafakari kwa ajili ya ukumbozi wetu,” amesema Pambalu.

Pambalu amesema amechukua hatua hiyo, ili kuwakomboa vijana na Watanzania kwa ujumla, kupitia Bavicha.

“Nimejipima nikaona katika siasa hizi za awamu ya tano, zinahitaji kijana jasiri dhidi ya siasa hizi za mabavu. Nina dhamira ya Kutatua changamoto za watanzania kupitia Bavicha, kwa kushirikiana na Chadema,” ameeleza Pambalu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Chadema: Samia aunde tume kuchunguza mauaji mgodi wa Barick

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ameombwa aunde tume huru kwa...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

error: Content is protected !!