Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Ofisi ya Msajili: Mkapa ana historia ndani ya CUF
Habari za Siasa

Ofisi ya Msajili: Mkapa ana historia ndani ya CUF

Sisty Nyahoza, Naibu Msajili wa Vyama vya Siasa nchini Tanzania
Spread the love

SISTY Nyahoza, Naibu Msajili wa Vyama vya Siasa nchini Tanzania amesema, Hayati Benjamin William Mkapa, Rais wa awamu ya tatu ameacha mchango wake ndani ya Chama cha Wananchi (CUF). Anaripoti Faki Sosi, Dar es Salaam … (endelea).

Akizungumza kwenye Mkutano Mkuu Maalum wa chama hicho ulioitishwa kwa ajili ya kupitisha majina ya wagombea urais Tanzania Bara na Visiwani Zanzibar leo Jumatatu tarehe 27 Julai 2020, Nyahoza amesema, miongoni mwa mambo aliyoanzisha Rais mstaafu Mkapa yaliinufaisha CUF.

Amesema, mwaka 1995, Rais Mkapa alianzisha ruzuku ya chama na kwamba, miongoni mwa vyama vya mwanzo kunufaika na ruzuku hiyo ni CUF.

“CUF ilianza kunufaika na mpango wa Rais Mkapa, lakini tulikuwa na tatizo la siasa Zanzibar, Rais Mkapa ndiye aliyesimamia na kutatua mgogoro huo kwa kusaini mkataba wa marudhiano. Sio hivyo tu, Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar uiliratibiwa na Rais Mkapa ndio maana nasema Mkapa ana historian a CUF,” amesema.

Pia, Nyahoza amesema, mpango wa Viti Maalum mwaka 2005 ulionzishwa na Rais Mkapa, CUF ni miongoni mwa vyama vya mwanzo vilivyonufaika.

Msajili huyo pia ameipongeza CUF kwa dhamira ya kufanya siasa za kistaarabu katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika tarehe 28 Oktoba 2020.

“Naipongeza CUF kwa kuamua kusimamia kauli ya kufanya kampeni kwa ustaarabu. Ninaamini mtasimamia kauli hiyo, lakini pia nampongeza Prof. Lipumba kwa kuandaa mkutano huu,” amesema Nyahoza na kuongeza “CUF bado ipo imara.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!