Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Nyuklia yazidi kumtesa Rais Trump 
Kimataifa

Nyuklia yazidi kumtesa Rais Trump 

Spread the love

RAIS wa Marekani Donald Trump amesaini sheria mpya ya kuongeza vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini juu ya mpango wake wa zana za Nyuklia kwa madi kwamba ni hatarishi kwa usalama wa taifa lake, anaandika Catherine Kayombo.

Kupitia Waziri wa Fedha wa Marekani, Trump ameidhinisha vikwazo hivyo  dhidi ya makampuni ya fedha yanayofanya biashara zake ndani ya Korea Kaskazini.

Ikiwa ni njia mojawapo ya kuyumbisha uchumi wa nchi hiyo katika biashara yake ya Nyuklia, rais wa Marekani amesema kuwa benki kuu ya China imeagiza taasisi za fedha kuacha kufanya biashara na Korea Kaskazini.

Hatua hiyo inakuja kufuatia agizo la Umoja wa Mataifa (UN) kuidhinisha vikwazo vipya dhidi ya taifa hilo kwa sababu ya jaribio lake la hivi karibuni la makombora ya masafa marefu.

Kufuatia jaribio hilo, hali ya wasiwasi imeendelea kutanda hasa nchini Marekani ambako majaribio kadhaa ya mwanzo yalielekezewa huko.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!