Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Michezo Nyota watatu wa Arsenal waongeza mkataba
Michezo

Nyota watatu wa Arsenal waongeza mkataba

Spread the love

WACHEZAJI wa klabu ya Arsenal Oliver Giroud 30, Laurent Koscielny 31 na Francis Conquelin 25, wameongeza mikataba yao ndani ya timu hiyo na kuendelea kuitumikia timu hiyo katika michuano tofauti.

Licha ya klabu ya Arsenal kutoweka wazi urefu wa mikataba hiyo, lakini Laurent Koscielny ambaye ni mmoja wa wachezaji waliosaini makubaliano mapya leo, aliandika kwenye ukurasa wake kupitia mtandao wa twitter kuwa ataendelea kusalia ndani ya timu hiyo mpaka 2020.

Nae kocha wa klabu hiyo Arsenal Wenger hakuwa nyuma kuwazungumzia wachezaji wake hao watatu kuwa wamekuwa na uzoefu kwa sasa na ni habari nzuri kwao baada ya kuongeza mkataba.

“Francis amepiga hatua kubwa kiufundi ndani ya uwanja, Olivier anauzoefu wa kutosha na Laurent amekuwa mtu muhimu kwenye kikosi chetu na naamini ni beki bora kwa sasa ulimwenguni” Wenger alisema.

Arsenal ambayo ipo nafasi ya tano kwenye ligi kwa sasa, inapitia katika kipindi kigumu kutokana na nyota wake Alexis Sanchez na Mesuit Ozil kutaka kuongezewa mshahara ili waendele kusalia kwenye kikosi hicho kutokana na mikataba yao kuwa ukingoni.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Piga pesa na mechi za EUROPA leo hii

Spread the love Hatimaye Alhamisi ya EUROPA imefika ambapo leo hii mechi...

Michezo

Leo ni leo nani kutinga nusu fainali UEFA?

Spread the love HATIMAYE Jumanne ya UEFA imefika ambapo leo hii michezo...

Michezo

Anza Jumatatu yako na Meridianbet

Spread the love  IKIWA ni siku nyingine mpya kabisa ya Jumatatu baadhi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC, Yanga wazindua kadi  za kimataifa za uanachama

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa kushirikiana na Klabu...

error: Content is protected !!