Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Michezo Nyota sita Spurs kuikosa Barcelona
Michezo

Nyota sita Spurs kuikosa Barcelona

Spread the love

KLABU ya Tottenham Hotspur ya Uingereza itawakosa wachezaji wake sita wa kikosi cha kwanza kuelekea kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya FC Barcelona utakaochezwa kesho kwenye Uwanja wa Wembely, London. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Wachezaji watakaoukosa mchezo huo wa kundi B ni Dele Alli, Mousa Dembele, Serge Aurier, Hugo Lloris, Christian Eriksen na mlinzi wa kati Jan Vertonghen ambao ni majeruhi.

Aurier ataendelea kukosekana baada ya kusumbuliwa na msuli wa nyuma ya mguu huku Dele Alli na Vertonghen wote watakuwa nje baada nao kupatwa na tatizo la misuli katika mchezo wa Ligi Kuu wiki iliyopita dhidi ya Huddersfield.

Kukosekana kwa wachezaji hao muhimu wa kikosi cha kwanza kwenye unaweza ukawa mtihani mgumu kwa kocha mkuu wa timu hiyo Mauricio Pochettino mbele ya mabingwa hao wa La Liga ambao nao hawakuwa na matokeo mazuri katika michezo miwili ya ligi iliyopita.

Spurs ambayo inakwenda kuvaana na Barcelona huku ikiwa na kumbukumbu ya kupoteza katika mchezo wao uliopita dhidi ya Inter Milan ya Italia, na kufanya kushika nafasi ya tatu kwenye kundi hilo huku ikiwa haina alama yoyote.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Tusua mkwanja na mechi za Ijumaa leo

Spread the love  LEO hii mechi zinaendelea kote na wewe kama unataka...

Michezo

Piga pesa na mechi za EUROPA leo hii

Spread the love Hatimaye Alhamisi ya EUROPA imefika ambapo leo hii mechi...

Michezo

Leo ni leo nani kutinga nusu fainali UEFA?

Spread the love HATIMAYE Jumanne ya UEFA imefika ambapo leo hii michezo...

Michezo

Anza Jumatatu yako na Meridianbet

Spread the love  IKIWA ni siku nyingine mpya kabisa ya Jumatatu baadhi...

error: Content is protected !!