Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Nusu ya wanafunzi vyuo vikuu wakosa mikopo
Elimu

Nusu ya wanafunzi vyuo vikuu wakosa mikopo

Mkurugenzi wa Idara ya Haki na Wajibu wa Wanafunzi Tanzania, Abdul Nondo
Spread the love

WANAFUNZI wa elimu ya juu wamezidi kuikaba koo  Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu  (HESLB), na kuitaka iwapatie mikopo, anaandika Faki Sosi.

Mtandao wa Wanafunzi wa Vyuo  Vikuu Nchini (TSNP), wametoa kilio hicho ikiwa ni siku chache tangu Rais John Magufuli kutangaza kwamba hakuna mwanafunzi wa elimu ya juu atakayekosa mkopo.

Juni 2  mwaka 2016  Rais Magufuli alisema hayo alipokuwa akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa maktaba ya kisasa ya chuo kuku cha Dar es Salaam (UDSM)  kampasi ya Mlimani.

Mkurugenzi wa Idara ya Haki na Wajibu wa Wanafunzi Tanzania,  Abdull Nondo ameomba serikali kuchukua hatua za dharura ili kuwapatia mikopo wanafunzi hao.

“Serikali ilichukulie suala hili kama dharua na kutoa mikopo kwa wanafunzi hawa wenye vigezo kama yalivyo mafuriko”

Nondo ameeleza kuwa wanafunzi wa mwaka wa kwanza  wametengewa fedha Sh. bilioni 108.8 ambapo HELSB imeeleza kuwa itatoa kwa wanafunzi 30,000  wakati waliomba wanafikia 61,000
Mmoja wa viongozi wa TSNP, Sity Ngwali ameeleza kuwa serikali inatakiwa kulipa kipaumbele suala hilo na kwamba  walitazame kwa jicho la tatu.

Wanafunzi hao walikusanyika leo katika ofisi za HESLB zilizoko Mwenge jijini Dar es Salaam hivyo kusababisha askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) kufika eneo hilo.

Baadhi ya wanafunzi waliangua vilio walipozungumzia shida  wanazopata kutokana na majina yao kutoonekana katika orodha ya wanaopata mikopo.

Mkurugenzi wa Mawasiliano wa HESLB, Omega Ngole amesema jukumu lao ni kuwapokea na kusikiliza hoja za wanafunzi hao kabla ya kuzifanyia kazi.

Amesema wamewataka wanafunzi hao kuorodhesha majina ili waangalie ni wapi walikosea na kuwapa majibu au kufanyia kazi changamoto zao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari za Siasa

Walimu 52,551 kupandishwa madaraja mwaka huu

Spread the loveNaibu Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala...

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanawake GGML wawanoa wanafunzi Kalangalala Sec. kujitambua

Spread the loveKATIKA kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanawake Duniani, Umoja wa...

error: Content is protected !!