Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Nondo aibua kikwazo mikopo Chuo Kikuu
ElimuTangulizi

Nondo aibua kikwazo mikopo Chuo Kikuu

Abdul Nondo, Mwenyekiti wa Ngome ya Vijana ACT-Wazalendo
Spread the love

MWENYEKITI wa Mtandao wa Wanafunzi Nchini (TSNP), Abdul Nondo amekitaja kikwazo kingine kwenye mikopo ya wanafunzi wa vyuo vikuu ni Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini Rita. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Nondo akizungumza na MwanaHALISI Online amesema kuwa Rita wamekuwa kikwazo kwa mikopo ya wanafunzi kutokana na kuchelewesha kuhakiki taarifa za vyeti vya kuzaliwa za wanafunzi.

Amesema kuchelewa kupitia na kuhakiki taarifa za wanafunzi  kunawanyima fursa ya kupata mikopo kutokana muda kuisha na kwamba dirisha la kuomba mikopo linafungwa Tarehe 15 Mwezi huu.

“Sisi kama Mtandao wa wanafunzi tumeiandikia barua Bodi ya Mikopo kuiomba waongeze muda wa kuomba mikopo kutokana na kuhofia wanafunzi wengi watakosa mikopo kutokana na ucheleweshwaji wa uhakika wa vyeti unaofanywa na  Rita,” amesema Nondo.

Amewatoa hofu wanafunzi waliomba mikopo kuwa hoja ya TSNP ina maslahi kwao hivyo itasikilizwa na kufanyiwa kazi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia kutunukiwa udaktari wa heshima Uturuki

Spread the loveBaraza la Chuo Kikuu cha Ankara, ambacho ni cha pili...

error: Content is protected !!