Wednesday , 24 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Njooni mnunue korosho-Serikali
Habari Mchanganyiko

Njooni mnunue korosho-Serikali

Spread the love

WIZARA ya Viwanda na Biashara kupitia taasisi yake ya Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade), imewataka wafanyabiashara, taasisi za umma na binafsi kujitokeza kununua korosho ghafi na zilizobanguliwa. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa tarehe 6 Aprili 2019 na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano TanTrade, Theresa Chambo, zoezi la uuzaji wa korosho hizo bado linaendelea.
Taarifa hiyo imewataka watu wenye nia ya kununua korosho ghafi na zilizobanguliwa kuwasilisha maombi ya katika mamlaka ya TanTrade, ikiwemo taarifa za kiasi cha korosho wanazohitaji.

“TanTrade inapenda kuwafahamisha kuwa, zoezi la uuzaji korosho linaendelea. Hivyo wafanyabiashara, wamiliki wa viwanda, hoteli, maduka ya jumla na rejareja, taasisi za umma na binafsi na wananchi kwa ujumla wenye nia ya kununua korosho wanakaribishwa kuwasilisha mahitaji yao,” inaeleza sehemu ya taarifa hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

Habari Mchanganyiko

Rufaa ya Equity Benki, State Oil yakwama

Spread the loveMAHAKAMA ya Rufani, jijini Dar es Salaam, imeshindwa kuendelea na...

Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the loveMADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaahidi kuendelea kuunga mkono Serikali za Mitaa

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya...

error: Content is protected !!