KIUNGO wa Simba Haruna Niyonzima amezua taharuki na hali ya sintofahamu kwa mashabiki na wapenzi wa klabu hiyo baada ya kutoonekana jana katika tamasha kubwa la ‘Simba Day’ ambalo mara nyingi hutumika kama jukwaa la kutambulisha kikosi kuelekea msimu mpya wa ligi kuu. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).
Katika tamasha hilo klabu ya Simba iliweka hadharani benchi la ufundi pamoja na wachezaji wake wote watakaotumikia timu hiyo katika michuano ya Ligi Kuu na Klabu Bingwa Afrika, katika msimu wa 2018/19 huku jina la Niyonzima likikosekana.
Huwenda kiungo huyo tayari ameshakuliwa hatua ya kinidhamu baada ya Kaimu Rais wa klabu ya Simba, Salim Abdallah alinukiliwa akisema kuwa kiungo huyo Mnyarwanda atachukuliwa hatua za kinidhamu kwa kuchelewa kurejea nchini kujiunga na timu baada ya ruhusa maalum aliyopewa kuisha.
Haruna ambaye alipewa ruhusa maalum na klabu yake hadi tarehe 20 Julai 2018, na alitakiwa arejee na kuungana na wenzake kwa safari ya Uturuki, lakini hakufanya hivyo licha ya taratibu zote za safari kukamilika lakini kutokana na kuchelewa alishindwa kwenda.