Tuesday , 23 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Watu wasiojulikana wafungua matairi gari la Lema
Habari MchanganyikoTangulizi

Watu wasiojulikana wafungua matairi gari la Lema

Spread the love

MBUNGE wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema amesema watu wasiojulikana walifungua baadhi ya nati kwenye taili ya gari yake kitu ambacho kingeweza kumsababishia ajali, anaandika Hamis Mguta.

Lema na Mbunge wa Arumeru mashariki (Chadema), Joshua Nassari walipanga kuondoka na gari hilo jana usiku kuelekea Dar es Salaam kuwasilisha ushahidi wa tuhuma za rushwa za madiwani waliohama Chadema ambapo kabla ya kuanza safari walibaini kuwapo kwa tatizo kwenye gari.

“Juzi nilisikia sauti isiyosawa tairi za nyuma nikapaki gari Equator Hotel. Dereva alipochukua gari tairi zote zikachomoka. Ninalindwa na Mungu.

“Tulibaini tairi za mbele wamefungua wakaacha wheelnut mbili mbili kila tairi, nyuma waliacha moja upande wa kushoto na kulia wakaacha mbili,” aliandika kupitia ukurasa wake wa Twitter.

Amesema kuwa baada ya kuhisi tatizo hilo aliliegesha katika hoteli ya Equator na baadaye kuomba msaada kwenye gari la Mwenyekiti wa Halmashauri ya Monduli, Isack Joseph kwenda naye Dar es Salaam.

“Asubuhi leo (Jumatatu) nikamtuma dereva wangu akachukue gari Equator hoteli alipeleke gereji na baada ya kutoka mita chache tairi zilichomoka,” amesema.

Amesema tayari amemuagiza dereva kwenda kutoa taarifa polisi lakini ameiomba kampuni ya ulinzi ya Inteligence inayolinda nyumba yake kufanya uchunguzi kubaini watu walioingia ndani na kufungua nati.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Watuhumiwa 12 wa kilo 726.2 za dawa za kulevya wafikishwa mahakamani

Spread the love  WATUHUMIWA watatu wamefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kibaha Mkoani...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari Mchanganyiko

GGML yasisitiza kuendelea kuimarisha afya za wafanyakazi

Spread the loveKAMPUNI ya Geita Gold Mining Limited kwa kushirikiana na kampuni...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!