Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Ni sarakasi, Polisi Vs Nondo, Daruso, LHRC
Habari za SiasaTangulizi

Ni sarakasi, Polisi Vs Nondo, Daruso, LHRC

Abdul Nondo, Mwenyekiti wa Ngome ya Vijana ACT-Wazalendo
Spread the love

BADO hakijaeleweka. Wakati Mawakili wa Kituo cha Haki za Binadamu (LHRC) na Serikali ya Wanafunzi ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Daruso) wakimsaka Abdul Nondo, Jeshi la Polisi bado halijataja alipo. Anaripoti Mwandishi wetu…(endelea).

Daruso na LHRC wamekuwa wakimtafuta Nondo ambaye ni Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi nchi (TSNP) ili kumwekea dhamana baada ya kuwa mikononi mwa Jeshi la Polisi zaidi ya wiki moja na nusu iliyopita, bado hawajafanikiwa. mpaka sasa Nondo hajapewa dhamana.

Taarifa za awali zinaonesha kuwa Nondo ameshikiliwa na Kituo Kikuu cha Kati cha Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam ambapo LHRC na Daruso walikwenda kufuatilia taratibu za kumwekea dhamana. Hata hivyo, walijibiwa hayupo kwenye kituo hicho.

Leo Mawakili wa LHRC, Jebra Kambole, Jones Sendodo na Reginard Martine ndio walioongoza safari ya kwenda kituoni hapo kwa lengo la kumwekea dhamana Nondo. Hata hivyo polisi walimweleza ‘hayupo hapa.’

Wakati wakiendelea kumsaka Nondo, jana Mawakili hao wa LHRC walifungua kesi ya kulitaka Jeshi la Polisi kumwacha Nondo au kumfikisha mahakamani kulingana na sheria za nchi zinazokataza mwananchi ama raia kuwekwa kituo cha polisi kwa zaidi ya saa 48.

Keshi hiyo itaanza kusikiliza kesho Machi 21 na Jaji Rehema Sameji. Kesi hiyo inalenga kulishikiza Jeshi la Polisi kumpeleka mahakamani au kumwamcha huru Nondo ambaye ni Mwanafunzo wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Wakili Jones ameuambia mtandao huu kwa njia ya simu kwamba walifika kituoni na kuelezwa kuwa, Nondo hayupo kituoni hapo.

“Tulienda kwenye Ofisi ya Kamanda Mambosasa (Lazaro Mambosasa-Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam), tumeambiwa yupo kwenye kikao.

“Tumepiga simu zake, hapokei. Hata hivyo, Kamanda Mambosasa amekuwa akitukwepa na kuwaambia waandishi kuwa sisi tunaishia mapokezi kitu ambacho sio cha kweli,’’ amesema Sendodo.

Amesema kuwa, mawakili wa LHRC wamekuwa wakipamba ili Nondo apate haki ya kikatiba ya kupata dhamana.

Taarifa zilizoufikia mtandao huu kuwa, uongozi wa (Daruso) chini ya Rais wake Jilili Jeremiah wamefika kituoni hapo na barua za kumdhamini Nondo bila mafanikio.

Vyanzo vyetu vya uhakika vimemuona Jilili na wenzake wakiwa kituoni hapo na barua za udhami ni kwa ajili kumdhamini Mwanafunzi mwenzao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!