Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa NEC yapigwa ‘stop’ kufanya haya
Habari za SiasaTangulizi

NEC yapigwa ‘stop’ kufanya haya

Spread the love

TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) nchini Tanzania haipaswi kufanya mambo makuu manne wakati wa mchakato wa Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Mambo hayo ni miongoni mwa Maadili ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani ya mwaka 2020.

Mambo hayo ambayo NEC haipaswi kufanywa ni; kupendelea chama chochote cha siasa au mgombea yeyote. Kubadili ratiba za kampeni za uchaguzi bila kushirikisha vyama vya siasa.

Pia, NEC haipaswa kuchelewa au kupeleka vifaa pungufu katika vituo vya kupigia kura bila sababu za msingi na mwisho kuchelewa kutangaza matokeo ya uchaguzi bila sababu za msingi.

Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC, Dk. Wilson Mahera

Katika maadili hayo, miongoni mwa mambo yanayotakiwa kufanywa na NEC ni kupanga, kusimamia na kuendesha uchaguzi katika misingi inayowezesha uchaguzi kuwa huru na wa haki.

Kuzingatia Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, sharia za uchaguzi na sharia nyingine za nchi;kuvipatia vyama vya siasa ratiba na taarifa za uchaguzi kwa wakati na kuratibu matumizi ya vyombo vya habari vya umma ili kutoa fursa sawa kwa wagombea urais na makamu wa Rais na vyama vyao.

NEC inaratibu kamati za kusimamia maadili ya uchaguzi pamoja na kusimamia utekelezaji wa maamuzi yanayotolewa na kamati hizo na kuandaa na kupeleka kwa wakati vifaa vya kutosha kwenye vituo vya kupigia kura.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!