Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa NEC yapuliza kipenga jimboni kwa Tundu Lissu
Habari za Siasa

NEC yapuliza kipenga jimboni kwa Tundu Lissu

Semistocles Kaijage, Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Tanzania (NEC)
Spread the love

TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imeeleza kuwa, uchaguzi mdogo katika Jimbo la Singida Mashariki utafanyika tarehe 28 Julai 28 mwaka huu. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Jimbo hilo lipo wazi tangu tarehe 28 Juni 2019 baada ya Job Ndugai, Spika wa Bunge kumvua ubunge Tundu Lissu (Chadema) kwa madai ya utoro na kutojaza fomu za maadili.

Katika taaifa iliyotolewa na Jaji Semistocles Kaijage, Mwenyekiti wa NEC leo tarehe 5 Julai 2019 imeeleza kuwa, uchaguzi huo unafanyika baada ya Spika Ndugai kuzingatia matakwa ya kisheria katika kumvua ubunge Lissu.

Ameeleza kuwa, amezingatia matakwa ya kifungu cha 37 (1) (b) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi katika sura ya 343.

Kifungu hicho kinamtaka kutoa taarifa kwa umma kusuhusu kuwepo wa uchaguzi mdogo wa ubunge katika kwenye jimbo hilo.

Akizungumza taratibu kuelekea uchaguzi huo Jaji Kaijage amesema, kwa kuzingatia Katiba ya nchi na Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, fomu za uteuzi wa wagombea zitatolewa kati ya tarehe 13-18 Julai 2019.

Na baada ya hapo amesea, uteuzi wa agombea utafanyika tarehe 18 Julai  2019 ambapo siku inayofuata, yaani tarehe 19-30 Julai 2019 kampeni zitakoma na tarehe 31 Julai 2019 uchaguzi utafanyika.

Kwenye taarifa yake hiyo, Jaji Kaijage amevikumbusha vyama vya siasa kuzingatia taratibu, sheria na kanuni za uchaguzi.

Wakati NEC ikitangaza uchaguzi huo, Lissu ambaye yupo Ubelgiji kwa matibabu baada ya kushambuliwa na risasi na watu wasiojulikana jijini Dodoma ameeleza dhamira yake ya kufungua kesi kupinga kuvuliwa ubunge wa jimbo hilo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!