Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa NEC yamteua Membe kugombea urais Tanzania  
Habari za Siasa

NEC yamteua Membe kugombea urais Tanzania  

Bernard Membe, Mgombea urais wa Tanzania kwa tiketi ya ACT-Wazalendo akirudisha fomu ya kuwania kiti hicho
Spread the love

TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), imemteua Bernard Membe kuwa mgombea urais wa Tanzania kupitia ACT-Wazalendo na mgombea mwenza, Profesa Omar Fakih Hamad kwenye Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Jumatano 28 Oktoba 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Membe na mgombea wake mwenza, Profesa Hamad wameteuliwa leo Jumanne tarehe 25 Agosti 2020 na Mwenyekiti wa NEC, Jaji Semistocles Kaijage katika ofisi za tume hiyo jijini Dodoma.

Membe aliyewahi kuwa waziri wa mambo ya nje wa Tanzania kati ya mwaka 2007 hadi 2015 enzi za utawala wa Rais mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete, amekuwa mgombea wa tisa kuteuliwa na tume hiyo.

Wagombea wengine waliokwisha rejesha fomu na kuteuliwa ni; Rais John Pombe Magufuli (CCM), Leopard Mahona (NRA), John Shibuda (Ada Tadea), Mutamwega Mgaiwa (SAU), Cecilia Augustino Mwanga (Demokrasia Makini), Yeremia Maganja (NCCR-Mageuzi), Ibrahim Lipumba (CUF)  na Philip John Fumbo wa DP.

Vyama vilivyojitokeza kuchukua fomu vilikuwa 17 na mpaka sasa vimerejesha tisa bado nane. Mwisho wa urejeshaji kwa mujibu wa NEC ni saa 10 jioni.

Endelea kufuatilia MwanaHALISI Online, MwanaHALISI TV na mitandao yetu ya kijamii kwa taarifa na habari mbalimbali

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!