Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa NEC kuzindua uandikishaji wapiga kura Julai 18
Habari za Siasa

NEC kuzindua uandikishaji wapiga kura Julai 18

Mwenyekiti wa NEC, Jaji Semistocles Kaijage
Spread the love

TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), inatarajia kuzindua Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura tarehe 18 Julai 2019 mkoani Kilimanjaro. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Kwa mujibu wa taarifa hiyo imetolewa leo na NEC, inaeleza kwamba Jaji Semistocles Kaijage, Mwenyekiti wa NEC amefungua mkutano wa wadau unaofanyika mkoani Kilimanjaro, ikiwa ni maandalizi ya uzinduzi rasmi wa daftari hilo.

Taarifa hiyo ya NEC imeeleza kuwa, miongoni mwa wadau wanaoshiriki katika mkutano huo ni pamoja na wawakilishi wa vyama vya siasa, viongozi wa dini, wawakilishi wa watu wenye ulemavu, vijana na asasi mbalimbali za kiraia.

Wakati huo, Jaji Mbarouk Salumu Mbarouk,  Makamu Mwenyekiti wa NEC amefungua mkutano wa wadau mkoani Arusha, pia mkutano huo umeshirikisha wadau kutoka vyama vya siasa, asasi za kiraia na watu wenye ulemavu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!