Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Ndumbalo ateuliwa kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje
Habari za SiasaTangulizi

Ndumbalo ateuliwa kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje

Spread the love

RAIS John Magufuli amemteua Mbunge wa Songea Mjini, Dk. Damas Ndumbaro kuwa Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, nafasi iliyokuwa inashikiliwa na Dk. Susan Kolimba. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Dk. Ndumbalo anachukua nafasi ya Dk. Susan ambaye uteuzi wake umetenguliwa.

Taarifa ya mabadiliko hayo imetolewa leo tarehe 26 Septemba 2018 na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu.

Vile vile, taarifa hiyo inaeleza kuwa, Rais Magufuli amemteua Dkt. Faraji Mnyepe kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akichukua nafasi ya Prof. Adolf Mkenda ambaye ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii.

Prof. Mkenda amechukua nafasi ya Meja Jenerali Mstaafu, Gaudence Milanzi ambaye amestaafu.

“Uteuzi wa viongozi hao umeanza leo tarehe 26 Septemba, 2018 na tarehe ya kuapishwa kwao itatangazwa baadaye,” inaeleza sehemu ya taarifa hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

Habari za Siasa

CCM yakemea ufisadi, yaipa kibarua TAKUKURU

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimekemea vitendo vya ubadhirifu wa...

Habari za Siasa

Bajeti ya Ikulu 2024/25 kuongezeka, bunge laombwa kurudhia Sh. 1.1 trilioni

Spread the love  WIZARA ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa...

error: Content is protected !!